NFRA Yaendesha mafunzo kwa Watumishi wake wa Ubora
Afisa Mtendaji Mkuu NFRA akagua mradi wa kuongeza uwezo wa Uhifadhi
KAMATI YA PAC YAKAGUA UJENZI WA MRADI WA KUONGEZA UWEZO WA KUHIFADHI NAFAKA UNAOJENGWA NA NFRA
Uzinduzi wa Ujenzi wa Magala na Vihenge
Jukumu kuu la Wakala ni kununua, kuhifadhi na kutoa chakula cha msaada katika maeneo yenye upungufu wa chakula na waathirika wa majanga mengine kitaifa. Wakala hutekeleza majukumu yake nchi nzima kupitia Kanda nane ambazo zimeundwa kimkakati kwa kuzingatia ukanda wenye uzalishaji mkubwa wa nafaka (Makambako, Songea, Sumbawanga na Songwe), Ukanda wenye uzalishaji wa wastani (Dodoma na Arusha) na ukanda wenye uzalishaji mdogo (Kipawa na Shinyanga).
Uanzishaji wa kanda hizi umewezesha Wakala kuhudumia mikoa yote ya Tanzania Bara ukiwa na maghala 34 yenye uwezo wa kuhifadhi tani 251,000.
Jedwali: Mgawanyo wa Mikoa Kikanda na Uwezo wa Kuhifadhi hapa chini.
Na.
Kanda
Uwezo wa Hifadhi (Tani)
Mikoa Inayohudumiwa
1
Arusha
39,000
Arusha, Kilimanjaro na Manyara
2
Dodoma
Dodoma na Singida
3
Kipawa
52,000
Dar es Salaam, Pwani, Tanga, Morogoro, Mtwara na Lindi
4
Makambako
22,000
Iringa, na Njombe
5
Shinyanga
14,500
Shinyanga, Tabora, Mwanza, Mara, Kagera, Geita, Simiyu na Kigoma
6
Songea
29,000
Ruvuma
7
Songwe
17,000
Mbeya na Songwe
8
Sumbawanga
38,500
Rukwa na Katavi
Jumla
251,000
Kuongeza Uwezo wa Kuhifadhi Nafaka
Wakala upo katika utekelezaji wa Mradi wa Kuongeza Uwezo wa Kuhifadhi nafaka katika kanda saba (7) mradi ambao ukikamilika utawezesha kuongeza uwezo wa kuhifadhi nafaka kutoka tani 251,000 zilizopo sasa kufikia tani 501,000.
Jedwali: Uwezo wa Kuhifadhi Nafaka wa sasa na Baada ya Kukamilika kwa Mradi
Uwezo wa Hifadhi kwa Sasa (Tani)
Uwezo wa Hifadhi Baada ya Mradi Kukamilika (Tani)
Mikoa ya Tanzania Bara
79,000
59,000
62,000
Iringa na Njombe
37,000
83,500
84,000
44,500
501,000