Majukumu

Majukumu

Ili kufikia dira na dhima, Wakala unatekeleza majukumu yafuatayo:-

i. Kuhifadhi akiba ya chakula toshelevu kwa mahitaji ya nchi;

ii. Kununua, kuhifadhi na kutoa akiba ya chakula ili kukabiliana na majanga;

iii. Kuzungusha na kutafuta masoko ya chakula ili kupunguza mfumuko wa bei na kuingiza mapato;na

iv. Kutoa huduma mbalimbali za uhifadhi ili kuongeza mapato.


Katika kutekeleza majukumu hayo, Wakala huweza kutumia vyanzo vifuatavyo vya Mapato:

i. Ruzuku kutoka Serikalini;

ii. Mauzo ya akiba ya chakula;

iii. Fedha zinazopatikana kutokana na huduma zinazotolewa na Wakala;

iv. Mikopo kutoka taasisi za fedha;

v. Misaada kutoka kwa washirika wa maendeleo.