Changamoto


Wakala unakutana na changamoto zifuatazo katika kutekeleza majukumu yake: -

1. Ufinyu wa bajeti ya kutekeleza Mpango Mkakati wa Wakala

2. Uchakavu wa baadhi ya Miundombinu ya uhifadhi;

3. Kupungua kwa uzalishaji wa nafaka katika baadhi ya misimu hivyo kusababisha kupanda kwa kasi kubwa kwa bei za kununulia akiba ya chakula;

4. Kushuka kwa bei za nafaka chini ya gharama za uzalishaji zinazoingiwa na mkulima pale uzalishaji mkubwa unapojitokeza hivyo kutishia kilimo endelevu.

5. Baadhi ya nafaka inayowasilishwa kuuzwa kwa Wakala kutokidhi vigezo vya ubora na hivyo kusababisha kasi ndogo ya ununuzi wa mahindi kwa baadhi ya Kanda.

Ufumbuzi wa Changamoto

1. Kutumia vizuri rasilimali zilizopo na kutafuta vyanzo vingine vya mapato kutekeleza mikakati yake;

2. Kuanza kukarabati baadhi ya miundombinu na kujenga miundombinu mipya kupitia mradi wa kuongeza uwezo wa kuhifadhi nafaka;

3. Kuboresha mbinu za ununuzi wa nafaka pale kunapojitokeza upungufu katika uzalishaji ;

4. Kununua mazao kwa bei inayorudisha faida kwa mkulima pale bei za nafaka zinaposhuka chini ya gharama ya uzalishaji, ili kuwezesha wakulima kuwa na kilimo endelevu.

5. Wakala kuendelea kuelimisha wadau mbalimbali wa Kilimo kuhusu uvunaji na utunzaji bora wa nafaka baada ya mavuno kwa kuzingatia vigezo vya ubora, ili kuweza kununua nafaka zenye kukidhi vigezo vya ubora.