Kanda ya Shinyanga

Ofisi za Kanda ya Shinyanga zipo katika Manispaa ya Shinyanga na inaongozwa na Meneja wa Kanda. Kanda ilianzishwa kimkakati ili kuweza kuhudumia Mikoa ya Kanda ya Ziwa ambayo ni Tabora, Shinyanga, Mwanza, Simiyu, Mara, Geita, Kagera na Kigoma. Kanda ya Shinyanga ina maghala yenye uwezo wa kuhifadhi tani 14,500 za nafaka.

Kwa sasa, Wakala inatekeleza mradi wa kuongeza uwezo wa kuhifadhi nafaka kwa kujenga vihenge na maghala ya kisasa ili kuboresha miundo ya uhifadhi katika eneo la Ibadakuli-Shinyanga mjini. Kukamilika kwa mradi huu kutawezesha kuongeza uwezo wa kuhifadhi nafaka kutoka tani 14,500 zilizopo sasa hadi tani 44,500.

Nafaka zinazonunuliwa, kuhifadhiwa na kuzungushwa/kuuzwa kupitia Kanda ya Shinyanga ni mahindi na mpunga. Kanda ya Shinyanga ni moja ya Kanda ambazo zinakuwa na uhitaji mkubwa wa nafaka katika masoko yake kutokana na kuwa na uzalishaji mdogo wa nafaka katika mikoa inayohudumiwa na kanda hii.

Mawasiliano;