Kanda ya Dodoma

Ofisi za Kanda ya Dodoma zipo katika Jiji la Dodoma na inaongozwa na Meneja wa Kanda. Kanda ilianzishwa kimkakati ili kuweza kuhudumia Mikoa ya katikati ya nchi ambayo ni Dodoma na Singida. Kanda ya Dodoma ina maghala yenye uwezo wa kuhifadhi tani 39,000 za nafaka, katika maeneo ya Kizota -Dodoma (tani 30,000), Manyoni -Singida (tani 4,500) na Singida Mjini (tani 4,500).

Kwa sasa, Wakala inatekeleza mradi wa kuongeza uwezo wa kuhifadhi nafaka kwa kujenga vihenge na maghala ya kisasa ili kuboresha miundo ya uhifadhi katika eneo la Kizota Kanda ya Dodoma. Kukamilika kwa mradi huu kutawezesha kuongeza uwezo wa kuhifadhi nafaka kutoka tani 39,000 zilizopo sasa hadi tani 59,000.

Nafaka zinazonunuliwa, kuhifadhiwa na kuzungushwa/kuuzwa kupitia Kanda ya Dodoma ni mahindi na mtama. Kanda hii huwa na uhitaji mkubwa wa nafaka.

Mawasiliano;