Kanda ya Arusha

Ofisi za Kanda ya Arusha zipo katika Jiji la Arusha na inaongozwa na Meneja wa Kanda. Kanda ilianzishwa kimkakati ili kuweza kuhudumia Mikoa ya Kaskazini ya nchi ambayo ni Kilimanjaro, Arusha na Manyara. Kanda ya Arusha ina maghala yenye uwezo wa kuhifadhi tani 39,000 za nafaka katika maeneo ya Themi (tani 39,000).

Kwa sasa, Wakala inatekeleza mradi wa kuongeza uwezo wa kuhifadhi nafaka kwa kujenga vihenge na maghala ya kisasa ili kuboresha miundo ya uhifadhi katika eneo la Makatani, Babati-Mkoa wa Manyara. Kukamilika kwa mradi huu kutawezesha kuongeza uwezo wa kuhifadhi nafaka kutoka tani 39,000 zilizopo sasa hadi tani 79,000.

Nafaka zinazonunuliwa, kuhifadhiwa na kuzungushwa/kuuzwa kupitia Kanda ya Arusha ni mahindi. Wakala pia huweza kununua mtama kupitia kanda ya Arusha pale kunapokuwa na uzalishaji mkubwa. Kanda hii imekuwa na soko kubwa la wanunuzi wa nafaka kutoka NFRA

Mawasiliano;